Wednesday, November 14, 2012

Waislamu Wanaamini Nini Kuhusu Yesu?

SWALI:
NATAKA KUJUA KUWA WAISLAMU MNAAMINI NINI HASA KUHUSU YESU?

JIBU:
Waislamu wanamheshimu na kumtukuzasana Yesu (‘Alayhis Salaam). wanamchukulia kuwa ni mmojawapo kati ya Mitume wakuu wa Mwenyezi Mungu kwa watu. Qur-aan inathibitisha kuzaliwa kwake na Bikira Maryam, na ipo Surah ya Qur-aan yenye jinaMaryam. Qur-aan inaeleza kuzaliwa kwa Yesu kama ifuatavyo: “Na pale Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu Anakubashiria (mwana)kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi ‘Iysa mwana wa Maryam, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa waliokaribishwa (kwa Mwenyezi Mungu). Naye atazungumza na watu katika utoto wake na katika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema. Maryam akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanaadamu? Mwenyezi Mungu Akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu Huumba Apendacho. Anapohukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa.” Qur-aan, 3:45-47)
Yesu alizaliwa kimiujiza kwa amri ya Mwenyezi Mungu ambayo ilimleta Aadam kuwa kiumbe pasina baba. Mwenyezi Mungu Amesema:
 Hakika mfano wa ‘Iysa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Aadam; Alimuumba kwa udongo kisha Akamwambia: Kuwa! Basi akawa.” (Qur-aan, 3:59)
Wakati wa mpango wake wa kiutume, Yesu alifanya miujiza mingi. 
Mwenyezi Mungu Anatuambia kuwa Yesu alisema: “Mimi nimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnacho kila na mnacho weka akiba katika nyumba zenu.” (Qur-aan, 3:49)
Waislamu wanaamini kwamba Yesu hakusulubiwa. Mpango wa maadui wa Yesu ulikuwa ni kumsulubu, lakini Mwenyezi Mungu Alimwokoa na Akamnyanyua Kwake. Mfano wa Yesu ukawekwa kwa mtu mwingine. Maadui wa Yesu walimchukua mtu huyu na wakamsulubu kwa kudhani alikuwa Yesu. Mwenyezi Mungu Amesema: “...Walisema: Sisi tumemuua Masihi ‘Iysa, mwana wa Maryam, Mtume wa Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsulubu, bali walifananishiwa tu...” Qur-aan, 4:157)
Si Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wala Yesu aliyekuja kubadili mafundisho ya msingi ya Dini ya kumwamini Mungu Mmoja, yaliyoletwa na Mitume waliotangulia, bali ni kuyathibitisha na kuyajadidisha.

Waislamu huamini pia kwamba Mwenyezi Mungu aliteremsha kitabu kitukufu kwa Yesu kiitwacho Injiyl, ambacho huenda sehemu yake ingalimo ndani ya Agano Jipya katika mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa Yesu. Hata hivyo, hii haimaanishi kuwa Waislamu wanaiamini Biblia tuliyo nayo katika zama hizi kwa sababu si maandiko ya asili yaliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu. Yamefikwa na mabadiliko, nyongeza na uondoshaji. Haya yalisemwa pia na Kamati iliyokuwa na majukumu ya kuipitia (na kuisahihisha na kuleta bora zaidi) The Holy Bible (Revised Standard Version). Kamati hii iliundwa na wasomi thelathini na wawili waliokuwa wajumbe wa Kamati hiyo. Walidhamini upitiaji na ushauri wa Bodi ya Ushauri yenye wawakilishi khamsini wa madhehebu shirikishi. Kamati ilisema katika Dibaji ya The Holy Bible (Revised StandardVersion), uk. iv: “Wakati mwingine kuna ushahidi dhahiri kuwa kitabu hiki kimepatwa na taabu ya upitishaji, lakini hakuna tafsiri yoyote kati ya hizo inayotoa utunzaji wa asili wa kutosheleza. Tunachoweza hapa ni kufuata tu, maoni yaliyo bora ya wasomi kama njia ya kufikia katika linayoelekea kuwa ndilo tengenezo jipya la andiko la asili.” Kamati hiyo ilisema tena katika dibaji, uk. Vii: “Nukuu zimeongezwa ambazo zinaonesha mabadiliko, nyongeza au uachaji wa msingi ndani ya mamlaka za kale (Mt 9.34; Mk 3.16, 7.4; LK 24.32, 52 n.k.).” Kuhusu maelezo zaidi juu ya mabadiliko ya Biblia, tafadhali tembelea www.islam-guide.com/bible]
                                                                                                                                  
The Aqsa Mosque in Jerusalem
(Tafadhali, tembelea www.islam-guide.com/pillars kwa ajili ya maelezo zaidi juu Yesu katika Uislamu.)

1 comment:

Animated Social Gadget - Blogger And Wordpress Tips Twitter Bird Gadget