Wednesday, November 14, 2012

Yesu ni Alfa na Omega?

SWALI:
Mbona nyie waislamu mnakataa kwama Yesu si Mungu wakati yeye anasema kuwa ni Alfa na Omega?

JIBU:
Ni kweli kuwa katika Kitabu cha Ufunuo 1, ayah ya 8, inaonyeshwa kuwa Yesu alisema yafuatayo kuhusu yeye mwenyewe: “Mimi ni Alfa na Omega”, asema Bwana, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja, Mwenye Nguvu”. Hizi ni sifa za Mwenyezi Mungu. Hivyo, Yesu, kulinagana na Wakristo wa mwanzo, hapa anadai uungu. 

Hata hivyo, hayo ni mojawapo ya maandiko yaliyo na makosa ya kiuchapishaji katika biblia za King James Version KJV.
-Katika 
RSV, wanazuoni wa Biblia walisahihisha tafsiri na kuandika: “Mimi ni Alfa na Omega”, asema Bwana Mungu, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja, Mwenye Nguvu”. 


-Masahihisho pia yalifanywa kwa New American Bible (Biblia Mpya ya Marekani) iliyochapishwa na Katoliki. Tafsiri ya Ayah hiyo imerekebishwa ili kuiweka katika muktadha wa sawa kaa ifuatavyo: “Bwana Mungu anasema: ‘Mimi ni Alfa na Omega, yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja, Mwenye Nguvu’”. 
Kwa masahihisho haya, ni dhahiri kuwa hii ni kauli ya Mwenyezi Mungu wala sio kauli ya Nabii ‘Iisa (YESU).

No comments:

Post a Comment

Animated Social Gadget - Blogger And Wordpress Tips Twitter Bird Gadget