Wednesday, November 14, 2012

Yesu alibatizwa? Na Je, Biblia Imeruhusu Ala Za Muziki Na Misalaba Kanisani

SWALI:
Je ni kweli Yesu Alibatizwa? Na Je, Biblia Imeruhusu Ala Za Muziki Na Misalaba Kanisani?


JIBU:Shukrani zetu za dhati kwa swali lako zuri japokuwa kufanya hivyo sio kuwa una dhamana ya uhakika kuweza kuwavuta Wakristo katika Uislamu. Biblia yenyewe tuelewe ina utata mkubwa katika mas-ala mengi hivyo kwa Mkristo aliyebobea huweza kukuvuruga wewe bila wasiwasi. Pia tufahamu hakuna kitabu kilichoteremshwa na Mwenyezi Mungu kinachoitwa Biblia.
Mas-ala mengi yana utata katika Biblia hivyo kuwachanganya hata wenye kuifuata Dini hiyo. Tukija katika suala lako twaweza kusema yafuatayo:
Ama kuhusu ubatizo wa Yesu Biblia inatueleza wazi kuwa alibatizwakama mistari ifuatayo inavyosema:
  1. "Mara tu Yesu alipobatizwa" (Mathayo 3: 16). Aliyembatiza ni Yohane kama ilivyo katika msitari wa 15 katika kitabu hicho cha Mathayo.
  2. "Yohane mbatizaji alitokea jangwani…Siku hizo, Yesu alitoka kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani" (Marko 1: 4 – 9).
  3. "Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa" (Luka 3: 21).
  4. Kitabu cha Yohane kinatueleza kuwa Yohane alikuwa anabatiza lakini hakumbatiza Yesu, kwani alishuhudia tu kuwa Yesu ni mwanakondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu (Yohane 1: 24 – 29).
Ama kuhusu vinanda na magitaa (ala za muziki) yapo mistari yanayoruhusu na mengine kukataza. Hilo linatuweka sisi katika hali ya utata kuwa ni lipi lililo sawa. Hebu tutazame baadhi ya maandiko:
  1. "Mwenyezi-Mungu asema hivi: 'Nazichukia na kudharau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini. Mjaponitolea sadaka zenu za kuteketezwa za nafaka, mimi sitakubali kuzipokea; na sadaka zenu za amani za wanono mimi sitaziangalia kabisa. Ondoeni mbele yangu kelele za nyimbo zenu! Sitaki kusikiliza muziki wa vinubi vyenu" (Amosi 5: 21 - 23). Tunaelezwa katika kitabu hicho hicho tena: "Nyinyi mnapenda kuimba ovyo na sauti ya vinubi na kubuni ala mpya za muziki mkimwiga mfalme Daudi" (Amosi 6: 5). Hizi ibara zinatuelezea nini sisi? Ibara ya awali inakataza muziki na ya pili inatuelezea kuwa kulikuwa kukibuniwa ala mpya za muziki kwa kumwiga mfalme Daudi. Je, ibara ya pili inaunga mkono muziki au inakataza? Kipengele kimoja kinakataza lakini cha pili kinaunga. Hili linatubabaisha zaidi kuhusu suala hili.
  2. Mistari ifuatayo inaruhusu suala hilo kwa uwazi kabisa. Hebu tutazame haya: "Mwimbieni kwa sauti Mungu, nguvu yetu mshangilieni Mungu wa Yakobo; vumisheni wimbo wa shangwe, pigeni ngoma, chezeni zeze na kinubi cha sauti nzuri. Pigeni tarumbeta kutangaza mwezi mwandamo, na pia mwezi mpevu, wakati wa sikukuu yetu" (Zaburi 81: 1 – 3). Hata hivyo, suala linakuja ni nani aliyeruhusu jambo hiloikiwa Zaburi 72: 20 inasema: "Mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese". Ikiwa ibara hii ndio mwisho wa Zaburi ya Daudi, sasa hii sura ya 81 inayoruhusu nyimbo na ala za muziki imeruhusiwa na nani? Bila shaka, itakuwa imeruhusiwa na mwingine na wala sio Daudi.
  3. Katika Agano la Kale tunaelezwa: "Kwa nini ulitoroka kisiri, ukanihadaa wala hukuniarifu ili nipate kukuaga kwa shangwe, nyimbo, matari na vinubi" (Mwanzo 31: 27). Ibara hii haiwezi kuchukuliwa kama ni ruhusa kwani aliyesema ni mshirikina ambaye katika msitari wa 32 amesema: "Lakini kwa nini uliiba vinyago vya miungu yangu?"
  4. Ruhusa nyingine inapatikana katika Kutoka 15: 20: "Basi nabii Miriamu, dada yake Aroni, akachukua kigoma mkononi, na wanawake wengine wote wakamfuata wakiwa na vigoma vyao wakicheza". Hii ni taarifa ya furaha iliyopatikana kwa upande wa wanawake pale Firauni alipoangamizwa na Mwenyezi Mungu wakiwa wanawake wapo peke yao.
Suala hili mbali na kuwa na utata dalili ya ibara zenye nguvu ni zile zinazokataza matumizi ya ala hizo.
Ama utumiaji wa msalaba katika kuvaa umezagaa kabisa kwa Wakristo wa zamani na wa sasa. Kufanya hivyo kwao ni kukumbuka kule kusulubiwa kwa Yesu kwa ajili ya dhambi za wanadamu nao waingie katika kusamehewa dhambi zao hapa duniani na kurithi uzima wa milele Siku ya Qiyaama. Hata hivyo, tukisoma katika Biblia tunapata kuwa Yesu hakusulubiwa kwani aliyesulubiwa atakuwa amelaaniwa. Hebu tutazame mistari ifuatayo:
  1. "Kama mtu amefanya kosa la jinai linalompasa auawe na akauawa kwa kutundikwa mtini" (Kumbukumbu la Sheria 21: 23).
  2. "Kristo alitukomboa kutoka katika laana ya sheria kwa kujitwalia laana hiyo kwa ajili yetu; maana Maandiko yanasema: 'Yeyote aliyetundikwa msalabani amelaaniwa" (Wagalatia 3: 13).
Hakika ni kuwa wenye kuamini kuwa Yesu kasulubiwa na misalaba kwa ajili ya kusamehewa dhambi wanapingana na Biblia. Hebu tusome mistari ifuatayo:
  1. "Maana ninachotaka kwenu ni upendo na si dhabihu, kumjua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa" (Hosea 6: 6).
  2. "Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: 'Nataka huruma, wala si dhabihu'. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi" (Mathayo 9: 13).
  3. "Kama tu mngejua maana ya maneno haya: 'Nataka huruma wala si dhabihu', hamngewahukumu watu wasio na hatia" (Mathayo 12: 7).
Kwa hivyo Yesu hakuja kuwa dhabihu, yaani kuuliwa msalabani bali amekuja kuwaokoa wenye hatia waingie katika mafundisho ya haki na hivyo kupata msamaha wa Mwenyezi Mungu.

Yesu ni Alfa na Omega?

SWALI:
Mbona nyie waislamu mnakataa kwama Yesu si Mungu wakati yeye anasema kuwa ni Alfa na Omega?

JIBU:
Ni kweli kuwa katika Kitabu cha Ufunuo 1, ayah ya 8, inaonyeshwa kuwa Yesu alisema yafuatayo kuhusu yeye mwenyewe: “Mimi ni Alfa na Omega”, asema Bwana, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja, Mwenye Nguvu”. Hizi ni sifa za Mwenyezi Mungu. Hivyo, Yesu, kulinagana na Wakristo wa mwanzo, hapa anadai uungu. 

Hata hivyo, hayo ni mojawapo ya maandiko yaliyo na makosa ya kiuchapishaji katika biblia za King James Version KJV.
-Katika 
RSV, wanazuoni wa Biblia walisahihisha tafsiri na kuandika: “Mimi ni Alfa na Omega”, asema Bwana Mungu, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja, Mwenye Nguvu”. 


-Masahihisho pia yalifanywa kwa New American Bible (Biblia Mpya ya Marekani) iliyochapishwa na Katoliki. Tafsiri ya Ayah hiyo imerekebishwa ili kuiweka katika muktadha wa sawa kaa ifuatavyo: “Bwana Mungu anasema: ‘Mimi ni Alfa na Omega, yule aliyeko na aliyekuwako na anayekuja, Mwenye Nguvu’”. 
Kwa masahihisho haya, ni dhahiri kuwa hii ni kauli ya Mwenyezi Mungu wala sio kauli ya Nabii ‘Iisa (YESU).

Waislamu Wanaamini Nini Kuhusu Yesu?

SWALI:
NATAKA KUJUA KUWA WAISLAMU MNAAMINI NINI HASA KUHUSU YESU?

JIBU:
Waislamu wanamheshimu na kumtukuzasana Yesu (‘Alayhis Salaam). wanamchukulia kuwa ni mmojawapo kati ya Mitume wakuu wa Mwenyezi Mungu kwa watu. Qur-aan inathibitisha kuzaliwa kwake na Bikira Maryam, na ipo Surah ya Qur-aan yenye jinaMaryam. Qur-aan inaeleza kuzaliwa kwa Yesu kama ifuatavyo: “Na pale Malaika waliposema: Ewe Maryam! Hakika Mwenyezi Mungu Anakubashiria (mwana)kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi ‘Iysa mwana wa Maryam, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa waliokaribishwa (kwa Mwenyezi Mungu). Naye atazungumza na watu katika utoto wake na katika utuuzima wake, na atakuwa katika watu wema. Maryam akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanaadamu? Mwenyezi Mungu Akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu Huumba Apendacho. Anapohukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa.” Qur-aan, 3:45-47)
Yesu alizaliwa kimiujiza kwa amri ya Mwenyezi Mungu ambayo ilimleta Aadam kuwa kiumbe pasina baba. Mwenyezi Mungu Amesema:
 Hakika mfano wa ‘Iysa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Aadam; Alimuumba kwa udongo kisha Akamwambia: Kuwa! Basi akawa.” (Qur-aan, 3:59)
Wakati wa mpango wake wa kiutume, Yesu alifanya miujiza mingi. 
Mwenyezi Mungu Anatuambia kuwa Yesu alisema: “Mimi nimekujieni na Ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na ninawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma, na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakwambieni mnacho kila na mnacho weka akiba katika nyumba zenu.” (Qur-aan, 3:49)
Waislamu wanaamini kwamba Yesu hakusulubiwa. Mpango wa maadui wa Yesu ulikuwa ni kumsulubu, lakini Mwenyezi Mungu Alimwokoa na Akamnyanyua Kwake. Mfano wa Yesu ukawekwa kwa mtu mwingine. Maadui wa Yesu walimchukua mtu huyu na wakamsulubu kwa kudhani alikuwa Yesu. Mwenyezi Mungu Amesema: “...Walisema: Sisi tumemuua Masihi ‘Iysa, mwana wa Maryam, Mtume wa Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsulubu, bali walifananishiwa tu...” Qur-aan, 4:157)
Si Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wala Yesu aliyekuja kubadili mafundisho ya msingi ya Dini ya kumwamini Mungu Mmoja, yaliyoletwa na Mitume waliotangulia, bali ni kuyathibitisha na kuyajadidisha.

Waislamu huamini pia kwamba Mwenyezi Mungu aliteremsha kitabu kitukufu kwa Yesu kiitwacho Injiyl, ambacho huenda sehemu yake ingalimo ndani ya Agano Jipya katika mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa Yesu. Hata hivyo, hii haimaanishi kuwa Waislamu wanaiamini Biblia tuliyo nayo katika zama hizi kwa sababu si maandiko ya asili yaliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu. Yamefikwa na mabadiliko, nyongeza na uondoshaji. Haya yalisemwa pia na Kamati iliyokuwa na majukumu ya kuipitia (na kuisahihisha na kuleta bora zaidi) The Holy Bible (Revised Standard Version). Kamati hii iliundwa na wasomi thelathini na wawili waliokuwa wajumbe wa Kamati hiyo. Walidhamini upitiaji na ushauri wa Bodi ya Ushauri yenye wawakilishi khamsini wa madhehebu shirikishi. Kamati ilisema katika Dibaji ya The Holy Bible (Revised StandardVersion), uk. iv: “Wakati mwingine kuna ushahidi dhahiri kuwa kitabu hiki kimepatwa na taabu ya upitishaji, lakini hakuna tafsiri yoyote kati ya hizo inayotoa utunzaji wa asili wa kutosheleza. Tunachoweza hapa ni kufuata tu, maoni yaliyo bora ya wasomi kama njia ya kufikia katika linayoelekea kuwa ndilo tengenezo jipya la andiko la asili.” Kamati hiyo ilisema tena katika dibaji, uk. Vii: “Nukuu zimeongezwa ambazo zinaonesha mabadiliko, nyongeza au uachaji wa msingi ndani ya mamlaka za kale (Mt 9.34; Mk 3.16, 7.4; LK 24.32, 52 n.k.).” Kuhusu maelezo zaidi juu ya mabadiliko ya Biblia, tafadhali tembelea www.islam-guide.com/bible]
                                                                                                                                  
The Aqsa Mosque in Jerusalem
(Tafadhali, tembelea www.islam-guide.com/pillars kwa ajili ya maelezo zaidi juu Yesu katika Uislamu.)

Krismasi ina Ushahidi wa Biblia?

SWALI:
Mimi ni mkristo nimekuwa nikiwauliza viongozi wangu wa kiriho lakini sipati jibu lenye hoja, na wengine huniambia kuwa katika dini yetu kuna "DOGMA" mengine hayaulizwi, ila mimi nahitaji kujua ukweli ili niwe huru.

Swali langu ni hili" Je, Krismasi ina ushahidi wa kibiblia? na je ni kweli Yesu alizaliwa 25 Desemba? Santa Claus (Baba Krismas) ni nani? Je Yesu na wanafunzi wake walishawahi kusheherekea Krismasi? Pia kama mtanipa historia ya krismasi ntafarijika sana.


JIBU:
Asante sana, lifuatalo ni jibu la maswali yako:
Historia ya Krismasi
Wakati wa zama za kale, siku ya mwisho ya majira ya baridi huko sehemu za Kusini kulisherehekewa mfano wa usiku ambao mungu wa Mama Watakatifu alijifungua mtoto akijulikana kuwa ni mungu wa Jua. Pia (siku hii) inaitwa Yule, siku ambayo inasherehekewa mno kwa kurushwa pashpashi. Ambapo kila mtu atacheza na kuimba ili kuliamsha jua kutokana na usingizi wake mnono wa majira ya baridi.
Wakati wa Warumi, iliadhimishwa kwa kumsifu Satunusi (mungu wa mavuno) na Mithrasi (mungu wa kale wa nuru), huo ni mtindo wa kuabudia jua ambao umekuja ukitokea Syria hadi Urumi. Karne kabla ya madhehebu ya Sol Invictus, ilitangaza ya kwamba, majira hayo ya baridi sio ya milele, na kwamba maisha yanasonga mbele, na ni mualiko wa kubaki kwenye nguvu nzuri.
Siku ya mwisho ya majira ya baridi huko sehemu za mviringo za Kusini ni baina ya siku ya 20 au 22 Disemba. Warumi waliadhimisha Saturnalia baina ya tarehe 17 na 24 Disemba.
Wakristo wa kale
Ili kuepuka kuchunguzwa wakati wa sherehe ambazo ni za wapagani, Wakristo wa kale walikaa majumbani mwao pamoja na mtakatifu Saturnalia. Kwa vile idadi ya Wakristo iliongezeka na mila zao zikaenea, sherehe zikachukua shuruti za Kikristo. Lakini, Makanisa ya kale hakika hayakusherehekea mwezi wa Disemba kwa kuzaliwa Kristo hadi alipokuja Telesforusi Telesphorus, ambaye alikuwa askofu wa pili wa Roma kutoka mwaka 125 hadi 136 AD, askofu huyo ndiye aliyetangaza kwamba huduma za Kanisa zifanywe wakati huu ili kuadhimisha “Kuzaliwa kwa Bwana wetu na Mwokozi”. Hata hivyo, kwa vile hakuna mtu hata mmoja aliye na uhakika wa mwezi ambao amezaliwa Kristo, kawaida ya Uzawa ulikumbukwa Septemba, ambao ulikuwa ni wakati wa Sherehe za Kiyahudi za Trumpetsi (kwa sasa ni Rosh Hashanah). Ukweli ni kuwa, kwa zaidi ya miaka 300, watu walielewa kuzaliwa kwa Yesu katika tarehe tofauti.
Katika mwaka 274 AD, kikomo cha jua kiliangukia tarehe 25 Disemba. Mfalme wa Roma aitwaye Aurelian alitangaza tarehe hiyo kama ni “Natalis Solis Invicti”, ‘Sherehe Ya Kuzaliwa Jua Lisiloshindikana’. Katika mwaka 320 AD, Papa Julius I aliitangaza tarehe 25 Disemba kama ni tarehe rasmi ya kuzaliwa Yesu Kristo.
Mnamo mwaka 325 AD, Krismasi ilitangazwa rasmi, lakini kiujumla haikutiliwa maanani. Mtakatifu Constantine, ambaye ni Mfalme wa mwanzo wa dhehebu la Ukristo la Kirumi, aliitanguliza Krismasi kama ni sherehe isiohamishika kwa tarehe 25 Disemba. Pia aliitanguliza Jumapili kama ni siku kuu ndani ya siku saba za wiki, na aliitanguliza (Pasaka) kama ni sherehe yenye kuhamishika. Mnamo mwaka 354 AD, Askofu Liberius wa Rumi, alitoa amri rasmi kwa wafuasi wake kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu ndani ya tarehe 25 Disemba.
Hata hivyo, ingawa Constantine aliifanya rasmi tarehe 25 Disemba kama ni sherehe ya kuzaliwa Kristo, Wakristo wakiitambua kama ni tarehe ya sherehe iliyofanana na mapagani, hawakushiriki katika mambo mazuri (kwa siku hii) iliyopangwa na Askofu. Krismasi ilishindwa kupata utambulisho wa kilimwengu miongoni mwa Wakristo hadi kipindi cha hivi karibuni. Huko Uingereza England, Oliver Cromwell alizipiga marufuku sherehe za Krismasi baina ya miaka 1649 na 1660 kupitia kwa inayoitwa Sheria za Rangi Samawati Blue Laws, akiamini kwamba iwe ni siku ya kumuabudu mungu tu.
Hamu ya kuifurahia sherehe ya Krismasi ilikirimiwa pale Waprotestanto (Wakristo wasiokubali baadhi ya mafundisho ya Kanisa la Kirumi) walipokimbia uchunguzi kwa kutorokea sehemu za makoloni yote duniani. Hata hivyo, Krismasi bado haikuwa ni sikukuu halali hadi miaka ya 1800. Na, weka akilini, hakukuwa na picha ya Baba Krismasi (Santa Claus) kwa wakati huo.
Krismasi inaanza kuwa maarufu
Umaarufu wa Krismasi ulianza ghafla mnamo mwaka 1820 kutokana na kitabu cha Washington Irving The Keeping of Christmas at Bracebridge Hall ‘Kuiadhimisha Krismasi Kwenye Jukwaa La Bracebridge’. Mnamo mwaka 1834, Malkia wa Uingereza aitwaye Victoria, alimkaribisha mumewe wa Kijerumani Prince Albert ndani ya Ngome ya Windso Windsor Castle, akimuonesha tamaduni za mti wa Krismasi Christmas tree na Nyimbo Za Kumsifu Yesu Kristocarols ambazo ziliadhimishwa Uingereza kwa Mfalme wa Uingereza. Mwaka 1834, wiki moja kabla ya Krismasi, Charles Dickens alichapisha Nyimbo za Kumsifu Yesu za Krismasi Christmas Carols(ambapo aliandika kwamba Scrooge alimuamrisha Cratchit kufanya kazi, na kwamba Baraza Kuu la Marekani US Congress lilikutana Siku ya Krismasi). Ilikuja kuwa ni maarufu mno hadi kufikia kwamba sio makanisa wala serikali kukana umuhimu wa sherehe za Krismasi. Mnamo mwaka 1836, Alabama ilikuja kuwa ni taifa la mwanzo ndani ya Marekani kutangaza Krismasi kama sikukuu halali. Mnamo mwaka 1860, mfananishi illustrator wa Marekani aitwaye Thomas Nast alichukua kutoka hadithi za Kiingereza kuhusu Mtakatifu Nicholas, muangalizi mtakatifu wa watoto, kumtengeneza Baba Krismasi Father Christmas. Mwaka 1907, Oklahoma ilikuwa ni ya mwisho miongoni mwa mataifa ya Marekani kutangaza Krismasi kama ni sikukuu halali. Mwaka baada ya mwaka, nchi za dunia nzima zilianza kuitambua Krismasi kama ni siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu.
Nakuombea Krismasi Njema Have a merry Christmas
Leo, mambo mengi yasiyokuwa ya Kikristo yananasibishwa ndani ya Krismasi. Yesu alizaliwa mwezi wa Machi, bado siku yake ya kuzaliwa inasherehekewa Disemba ya 25, wakati wa solstice. Sherehe za Krismasi zinamalizikia siku kumi na mbili za Krismasi (Disemba 25 hadi Januari 6), ni idadi hiyo hiyo ya siku ambazo zilisherehekewa na wapagani wa ki-Rumi wakale kwa kuadhimisha kurudi kwa jua. Hivyo, hakuna mshangano wowote kwamba Wakristo waliosafi puritans – au Wakristo wasiotaka mabadilikoconservative – watahamaki kwa Krismasi kuwa “sio ya kidini kama ilivyotakikana kuwa,” wakisahau kwamba Krismasi haikusherehekewa hata kidogo hadi siku za hivi karibuni.
Yesu Alisemaje Kuhusu Krismasi?
Mazoea ya Krismasi
Mti ulio bora wa Krismasi unanunuliwa. Ukipambwa kwa madoido yenye kung’ara pamoja na kumetameta, unasimamishwa karibu na dirisha. Maduka yanajazana wanunuzi wakisaka zawadi na vile viduchu vinasubiri kwa hamu kubwa ya Baba Krismasi Santa.
Ni mshughuliko na ni homa ya Krismasi Christmas fever, umewahi kufikiri kabla? Je, Biblia au Yesu aliwahipo kusababisha homa ya Krismasi?Tafakari juu ya mchanganuo ufuatao kuhusu Krismasi, na ukweli utakuja kuwa wazi zaidi na zaidi.
Je, Krismasi Ina Ushahidi wa Biblia?
Neno ‘Krismasi’ halipo ndani ya Biblia. Biblia ilifunga midomo ya sherehe yote inayohusiana na Krismasi, isipokuwa kwa kitu kimoja; upambaji wa mti. Biblia wenyewe inashutumu upambaji wa miti (ya Krismasi):
“Mila za watu si chochote, wanakata mti kutokana na msitu, na mchongaji anauchonga kwa patasi yake, wanaupamba kwa fedha na dhahabu, wanaugandanisha kwa nyundo na misumari ili usipate kutikisika” (Jeremia 10-3,4).
Wazungu wa ki-Pagani kabla ya Ukristo, waliamini miujiza kwamba miti ya kijani ina nguvu maalum za ulinzi. Hakika, matumizi ya Miti ya Krismasi imeanza hivi karibuni tu mwa karne ya 17 hukoStrasbourg, Ufaransa na kutoka huko ukaenea hadi Ujerumani, Uingereza na baadaye Marekani. “Ibada ya miti ilikuwa ni jambo la kawaida kwa dini miongoni mwa watu wa Tyutoniki Teutonic na Skandinavia Scandinavia wa Ulaya ya kaskazini kabla ya kuingia kwenye Ukristo…Walowezi wa ki-Jerumani walileta mila za Mti wa Krismasi kwenye makoloni ya Kimarekani mnamo karne ya 17. Kufikia karne ya 19, matumizi yake yalienea sehemu tofauti”. (Angalia Encyclopedia ya Compton, Toleo la 1998)
Je, Yesu Alizaliwa Disemba ya 25?Si tarehe ya Disemba 25 wala tarehe nyengine yoyote iliyotajwa ndani ya Biblia kuhusu kuzaliwa kwa Yesu. Ilikuwa ni hivyo hadi kufikia mwaka 530 C.E kwamba mtawa monk aitwaye Dionysus Exigus, aliweka tarehe isiyobadilika ya kuzaliwa kwa Yesu kuwa ni Disemba 25. “Kulingana na taratibu za ki-Roma, alikosea kuipanga tarehe ya kuzaliwa kwa Kristo (yaani, miaka 754 baada ya kupatikana nchi ya Rumi) kama ni Disemba 25, mwaka 753”. (Angalia: Encyclopedia Britannica, toleo la mwaka 1998) Tarehe hii ilichaguliwa ili iendane pamoja na sikukuu ambazo zimeshagandana na imani za kipagani.
Mapagani wa Kirumi walisherehekea Disemba 25 kama ni ya kuzaliwa kwa ‘mungu’ wao wa nuru, aitwaye Mithra.
“Mnamo karne ya pili A.D, hiyo sherehe ya Mithra ilikuwa ni ya kawaida zaidi ndani ya Ufalme wa Rumi kuliko Ukristo, ambayo ilizaa mifanano iliyo mingi” (The Concise Columbia Encyclopedia, toleo la mwaka 1995).
‘Waungu’ wengine wakipagani waliozaliwa Disemba ya 25 ni: Hercules mtoto wa Zeuz (Wagiriki); Bacchus, ‘mungu’ wa mvinyo (Warumi); Adonis, ‘mungu’ wa Kigiriki, na ‘mungu’ Freyr wa Ugiriki-mapagani wa Roma.
 Je, Vipi Kuhusu Baba Krismasi Santa Claus?
Kama viumbe visivyokuwa binaadamu aliens watafika duniani katika wakati wa Krismasi, bila ya shaka wataamini Krismasi kuwa ni sherehe ya kufurahikia kuzaliwa kwa Baba Krismasi Santa. Majina ya ‘Santa Claus’, hayamo popote ndani ya Biblia.
Hata hivyo, Mtakatifu Nikolas Saint Nicholas (Baba Krismasi Santa Claus) alikuwa ni mtu halisi, askofu, ambaye alizaliwa miaka 300 baada ya Yesu. Kwa mujibu wa hekaya za kale, alikuwa ni mtu mwenye huruma mno na alitenga nyakati za usiku kwenda kutoa zawadi kwa mafukara. Baada ya kifo chake mnamo Disemba ya 6, watoto wa shule huko Ulaya walianza kusherehekea siku hiyo kwa karamu kila mwaka.
Baadaye Malkia Victoria aliibadilisha sherehe hiyo kutoka Disemba ya 6 kuwa ni Disemba ya 24 kuamkia Krismasi.
Je, Yesu au Wafuasi Wake Waliwahi Kusherehekea Krismasi?Kama Yesu alimaanisha kwa wafuasi wake kusherehekea Krismasi, angeliifanyia kazi yeye mwenyewe na kujikusanya pamoja na wafuasi wake. Hakuna sehemu iliyotajwa ndani ya Biblia kwamba kuna mfuasi yeyote aliyewahi kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu kama Wakristo wanavyofanya leo.
“Kanisa halikupatapo kuweka sikukuu kwa ajili ya sherehe za tukio la Krismasi hadi ilipofika karne ya 4” (Angalia: Encyclopedia ya Grolier)
Hivyo, tunaona kwamba sio Biblia wala Yesu na wafuasi wake waliosema kitu kuhusu sherehe za Krismasi ambazo sasa zinahusisha viingilio vya sherehe, biashara, na matumizi yaliyochupa mpaka, ni utovu wa akili kwa mfananisho wowote wa imani.

Tuesday, November 13, 2012

Naomba ushahidi wa utume wa YESU (A.S)..

SWALI:
Hello "Majibu Yetu",

Mimi ni mkristo lakini huwa nasikia mkisema kuwa Yesu ni mtume tuu na kuna rafiki yangu mwislamu alinionesha kwenye kitabu chenu katika 5:75 kuwa Yesu si chochote ila ni Mtume tuu, na wamekwishapita mitume kabla yake.

Swali langu ni hili"Naomba ushahihi wa  Biblia kuwa Yesu alitumwa."


JIBU:
Asante sana kwa swali lako.
Kwa kweli yapo maandiko mengi sana katika Biblia yanayothibitisha kuwa Yesu (Amani iwe naye) ni mtume tu.

Haya hapa chini baadhi tuu ya maandiko hayo:
YOHANA 5:24    
"Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima.

YOHANA 5:30
     "Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi nina hukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma.

 YOHANA 5:36
     Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma.

 YOHANA 5:37
     Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake.
       
YOHANA 7:16
     Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.

YOHANA 7:28
     Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.

YOHANA 7:29
     Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."

YOHANA 7:33
     Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
       
YOHANA 8:16
     Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.

YOHANA 8:18
     Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia."

YOHANA 8:26
     Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake."

YOHANA 8:29
     Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza."
       
YOHANA 6:38
     kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.

YOHANA 6:39
     Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
       
YOHANA 12:44
    Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, "Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.

YOHANA 12:49
    Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
       
MATAYO 10:40
   "Anayewakaribisha ninyi, ananikaribisha mimi; na anayenikaribisha mimi, anamkaribisha yule aliyenituma.
       
MARKO 9:37
       "Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma."
       
LUKA 9:48
  akawaambia, "Mtu yeyote anayempokea mtoto huyu mdogo kwa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma. Maana yule aliye mdogo kuliko wote kati yenu ndiye aliye mkubwa kuliko wote."
       
LUKA 10:16
        Halafu akasema, "Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma."
       
YOHANA 4:34
     Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
       
YOHANA 9:4
       Kukiwa bado mchana yatupasa kuendelea kufanya kazi za yule aliyenituma; maana usiku unakuja ambapo mtu hawezi kufanya kazi.
       
YOHANA 13:20
    Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma."
       
YOHANA 14:24
    Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno mlilosikia si langu, bali ni lake Baba aliyenituma.
       
YOHANA 15:21
    Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma
.
       
YOHANA 16:5
     Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: `Unakwenda wapi?`

Friday, October 26, 2012

Hutba ya mwisho ya Mtume!!

Swali:
Assalaam aleykum,Mimi ni mwislamu na naomba mnijuje hutba ya mwisho ya Mtume (S.A.W).

Jibu:
Kila nikiisoma khutba hii huhisi kama imetolewa jana wakati ni karne kumi na nne na thuluthi (miaka 1427) tayari zimepita. Kila nikiisoma khutba hii huyatafakari tena maneno haya machache ya Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) lakini yamejaa mafundisho na kusheheni hazina ya elimu na mausio . Khutba iliyokusudiwa waislamu wote duniani popote walipo, kizazi baada ya kizazi ,karne baada ya karne. Ni wosia ambao ametuagiza Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) tuufikishe kwa kila muislamu.

Khutba hii ilitolewa na Mtume Muhammad (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) tarehe 09 Dhul Hijja mwaka wa 10 Hijriya kwenye Mlima Arafah huko Makkah – Saudi Arabia - alipokwenda Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) kufanya ibada ya Hijja ambayo pia ilijulikana kama Hijja ya kuaga. Baada ya kumshukuru Allah (Subhaanahu Wata’ala) na kumsifu, Mtume (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) alianza khutba kwa kusema:
---
“ Enyi watu! Nisikilizeni maneno yangu vizuri , kwani sidhani kama baada ya mwaka huu nitakuwa pamoja nanyi. Hivyo sikilizeni kwa makini nitakayoyasema na (maneno haya ) mfikishieni kila asiekuwepo hapa leo.”

“Enyi watu! Hakika damu zenu na mali zenu ni takatifu kwenu kama mlivyoufanya mwezi huu kuwa mtakatifu na mji huu kuwa mtukufu .
”Rudisheni amana mlizokabidhiwa kwa wenyewe wanaostahiki . Msimdhuru yeyote ili nanyi msije mkadhuriwa . Kumbukeni mtakuja kukutana na mola wenu naye atahesabu amali zenu. Allah (Subhaanahu Wata’ala) amekukatazeni kula riba . Hivyo riba zote zimeondoshwa na mna haki ya kubaki na rasilmali (mitaji) yenu . Hamna haki ya kudhulumu wala kudhulumiwa . Allah (Subhaanahu Wata’ala) ameharamisha riba na riba zote za Abbaas ibn Abdul Muttallib zimeondoshwa ”

Kila haki ya kisasi iliyekuwepo enzi za Ujahiliya imefutwa na haki ya kwanza kuifuta ni ya Rabiah ibn Harith ibn Abdul Muttalib “

“Enyi watu! washirikina wanajaribu kuakhirisha (kuchelewesha) kalenda ili wafanye kuwa Salla Allahu ‘Alayhi Wasallama idadi ya ile (miezi) aliyo itukuza Allah na kulifanya halali jambo ambalo Allah(Subhaanahu Wata’ala) ameliharamisha na kulikataza jambo ambalo Allah(Subhaanahu Wata’ala) ameliruhusu . Miezi kwa Allah(Subhaanahu Wata’ala) ni kumi na miwili . Mine kati yao ni mitakatifu, mitatu ikiambatana (Dhul Qaadah, Dhul Hijjah na Muharram) na mmoja (Rajab) uko kati ya Jumada (ya mwanzo na ya mwisho) na Shaaban.
“Jiepusheni na shetani kwa ajili ya kuilinda dini yenu . Tayari (shetani ) amekata tamaa kwamba ataweza kuabudiwa katika ardhi hii milele lakini bado ana mikakati ya kukupotezeni hivyo tahadharini nae katika mambo mengine .”

“Enyi watu ! ni kweli mna haki juu ya wanawake na wao pia wana haki juu yenu . Kumbukeni mmewachukua kuwafanya wake zenu kwa amana ya Allah(Subhaanahu Wata’ala) na mmehalalishiwa (kustarehe) nao kwa neno lake” . “Nnakuusieni kuwatendea wema wanawake na kuwa na huruma kwao kwani ni wake zenu na wasaidizi wenu .Ni haki yenu kuhakikisha hawafanyi urafiki na msiyemuafiki na ni juu yao kutokufanya jambo la uchafu lililo wazi na pindipo wakifanya Allah amewapa idhini ya kuwahama kwenye malazi na kuwapiga kipigo kisichoumiza. Ikiwa watatekeleza majukumu yao basi na wao watakuwa na haki ya kulishwa na kuvishwa kwa wema.”
“ Enyi watu, nisikilizeni kwa utulivu , mcheni Allah(Subhaanahu Wata’ala) , msali sala tano kila siku, fungeni katika mfungo wa Ramadhan na toeni Zakah. Tekelezeni ibada ya Hijjah ikiwa mna uwezo.”

“ Binadamu wote wametokana na Adam na Hawaa , hakuna mbora kati ya mwarabu na asiyekuwa mwarabu , wala asiekuwa mwarabu kwa mwarabu , wala mweupe kwa mweusi au mweusi kwa mweupe isipokuwa kwa Taqwa( kumcha Allah).
“Eleweni kila muislamu ni ndugu kwa muislamu na waislamu wote ni ndugu. Hatohalalishiwa muislamu kitu chochote isipokuwa kila alichopewa kwa ridhaa na ndugu yake . Wala msidhulumu nafsi zenu . Na msisahau kwamba kuna siku mtakutana na mola wenu na mtahesabiwa amali zenu. Hivyo tahadharini msije mkapotea baada yangu”
“Enyi watu ! Hakuna tena Mtume baada yangu na hakuna dini nyengine itakayokuja. Ninakuachieni vitu viwili ambavyo mkishikamana navyo hamtopotea milele navyo ni QURAAN na SUNNA (mwenendo) zangu.”
“Wale wote walionisikiliza waufikishe ujumbe huu kwa wengine, na wengine waufikishe kwa watakaofuatia na inawezekana hawa wa mwisho wakayafahamu vyema maneno yangu kuliko hawa walionisikiliza moja kwa moja.”

“Ewe mola shuhudia kwamba nimefikisha ujumbe kwa watu wako”

Ndugu zangu waislamu, hazina kama hizi ndizo tulizoagizwa kufikishiana. Inshaallah kila atakaepata ujumbe huu ahakikishe anamfikishia mwengine kama tulivyoagizwa na Al Habib Mustafa (Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) na asaa inawezekana miongoni mwetu kuwapata tutakaomsikiliza Mtume(Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam) na kumfahamu vyema na hivyo kuufuata mwenendo wake . Tumuombe Allah(Subhaanahu Wata’ala) atujaalie miongoni mwao. Amin

Saturday, October 6, 2012

Jina la Tanzania lilitungwa na mwislamu?

Swali:
Hello, mimi naitwa Getruda naishi zanzibar.
Swali langu ni "eti ni kweli jina la Tanzania liliundwa na mwislamu?"

JIBU:
Ni kweli kabisa.Anaitwa Mohammed Iqbal na kwa sasa anaishi uingereza.

Huyu bwana aliyebuni jina la Tanzania ni Muhindi na Dini yake ni AHMADIYA MUSLIM JAMAAT TANZANIA majina yake ni MOHAMMED IQBAL DAR.
Mohammed alizaliwa Mkoani Tanga miaka ya 1944, Baba mzazi wa Mohammed alikuwa Daktari huko mkoani Morogoro alikuwa anaitwa Dkt. T. A. DAR  alikuwa Tanganyika kuanzia mwaka 1930.

Mohammed Iqbal Dar alipata elimu yake ya Msingi Mkoani Morogoro shule ya Msingi H H D AGHAKHAN kwa sasa ni Shule ya Serikali na baada ya hapo alikuja baadae kujiunga na Chuo cha Mzumbe akasoma Kidato cha Kwanza mpaka cha Sita.


Mohammed anasema alikuwa Maktaba akijisoma gazeti la Tanganyika Standard, siku hizi Daily News, akaona Tangazo linasema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unafahamika kama Republic of Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana refu sana kwa hiyo Wananchi wote wakaombwa Washiriki kwenye shindano la Kupendekeza jina moja litakalo zitaja nchi zote mbili yaani Tang
anyika na Zanzibar Mohammed Iqbal Dar anasema aliamua kuingia kwenye Shindano na hivi ndivyo alianza Safari ya Kubuni Jina la Muungano.

Kwanza anasema alichukua karatasi akaandika Bismillah Raahman Rahimu hii ni kutokana na Imani yake na baada ya hapo akaandika jina la Tanganyika baada ya hapo akaandika Zanzibar halafu akaandika jina lake Iqbal halafu akaandika jina la Jumuiya yake ya Ahmadiya baada ya Hapo akamrudia tena Mwenyezi Mungu akamwomba amsaidie ili apate jina zuri kutoka katika majina hayo aliyokuwa ameyaandika. Baada ya hapo Mohammed Iqbal Dar alichukua herufi tatu kutoka Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar akachukua Herufi tatu za Mwanzo ZAN ukiunganisha unapataTANZAN alivyoona hivyo akachukua I herufi ya kwanza katika jina lake la Iqbal na akachukuaA kutoka jina la dini yake yaani Ahmadiyya kwa maana hiyo ukiongeza herufi hizi mbili I na Akwenye TANZAN unapata jina kamili TANZANIA akalisoma jina akaliona ni zuri lakini akajiridhisha pia kwamba akiongeza herufi hizo za I na A kwenye TANZAN italeta maana kwakuwa nchi nyingi za Afrika zinaishia na IA, mfano EthiopIA, ZambIA, NigerIA, TunisIA, SomalIA, GambIA, NamibIA, LiberIA, MauritanIA alivyoona hivyo akaamua apendekeze kuwa jina TANZANIA ndio litumike kuwakilisha nnchi hizi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar kwa maana hiyo jina TANZANIA limezaliwa kutoka majina manne majina hayo ni Tanganyika, Zanzibar, Iqbal na Ahmadiyya.

Mohammed Iqbal Dar baada ya kupata jina hilo akalituma jina hilo kwenye kamati ya kuratibu Shindano. Baada ya Muda mwingi kupita baba yake na Mohammed Iqbal Dar alipokea barua nzito kutoka Serikalini ikiwa inasomeka kama ifuatavyo…

REPRESENTED BY THE
MINISTRY OF INFORMATION AND TOURISM, TANZANIA
TO
MOHAMED IQBAL DAR
IN RECOGNATION OF THE ACHIEVEMENT OF CHOOSING THE NEW NAME FOR THE
UNITED REPUBLIC OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR NAMELY
“REPUBLIC OF TANZANIA”
DURING THE NATIONAL COMPETITION DAY IN 19TH NOVEMBER 1964
I A WAKAL
MINISTER FOR INFORMATION AND TOURISM

Barua hiyo pia ilisema...

“Utakumbuka kuwa miezi michache iliyopita ulituandikia kutupa ushauri kuhusu jina jipya la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na wewe pamoja na wananchi wenzio 16 ulishauri nnchi yetu iitwe Tanzania. Nafurahi kukuarifu kuwa mshirikiane ile Zawadi ya sh. 200 iliyoahidiwa na leo nakuletea check ya sh. 12/50 ikiwa ni hisa yako katika zile sh.200. Nashukuru sana kwa jitihada ya kufikiri jina la Jamuhuri yetu.”

Barua ikasainiwa na Idrisa Abdul Wakil aliyekuwa Waziri wa Habari na utalii wakati huo.

Sasa kwa nini Mohamedi Iqbal Dar anadai yeye kuwa mshindi pekee wakati barua ilikuwa inaonyesha kulikuwa na washindi wengine 15 ambao nao walishinda?

Jibu ni kuwa wakati wa kutolewa kwa zawadi hizo hakuna aliyejitokeza zaidi ya Bwana Mohammed Iqbal Dar na Bwana Yusufal Pir Mohamed ambaye hata hivyo alikosa sifa baada ya kushindwa kutoa barua ya kumpongeza kuwa ameshinda kwa madai kuwa Barua ameipoteza, hivyo Wizara ya Habari na Utalii iliamua kumtangaza Mohammed Iqbal Dar kuwa Mshindi na kumpatia zawadi yote ya sh.200/; pamoja na Ngao.

Bwana Mohammedi Iqbal Dar anasema anachosikitika ni kuwa mchango wake bado Watanzania hawathamini mchango wake lakini yeye anaipenda Tanzania na anajivunia kuwa Mtanzania japo anadhani dini yake ya Uislamu ndiyo tatizo hawataki kutambua mchango wake ila anaamini kuwa siku moja ukweli utajulikana.

Hayo ni maelezo ya Mohammed Iqbal ambaye kwa sasa anaishi Uingereza kwa kuwa huko ndiko alipata kazi eneo la Birmigham b35 6ps UK, Dar– es-Salaam House, 18 TURNHOUSE 
ROAD, PHONE 44 121-747-9822


Wednesday, July 11, 2012

Kaa & Kamba ni halali?

Swali: 
Waislamu tunaruhusiwa kula Kaa na Kamba wa baharini?


Jibu:
MwenyeziMungu anasema;5:96. Nyinyi mmehalalishiwa kuvua vinyama vya baharini na kuvila, kwa faida yenu na kwa wasafiri...

Kutokana na aya hiyo ni kwamba wanyama wapatikanao baharini ni halali.

Wapo wanaosema kuwa KAA (Crab) ni haramu lakini mpaka sasa hatujapata ushahidi wowote kutoka katika Quran & Hadithi sahihi kuharamisha ulaji wake.

Thursday, July 5, 2012

Are there hadiths about cutting beards?

Question: Asalaam Aleykum, Am a muslim and my question is "Are there hadiths about cutting beard and trimming mustaches?"


Answer: 
Yes, here in below are some of the requested hadiths;





TIRMIDI (2772)
قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَحْفُوا الشَّوَارِبَ وَأَعْفُوا اللِّحَى

Sayyidina Ibn Umar (RA) reported that Allah’s Messenger (SAW) said, “Cut the moustache and grow beard.”

TIRMIDI (2773)
أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَمَرَنَا بِإِحْفَاءِ الشَّوَارِبِ وَإِعْفَاءِ اللِّحَى

 Sayyidina Ibn Umar (RA) reported that Allah’s Messenger (SAW) gave the command to cut the moustache well and to grow the beard.
Dawud :: Book 1 : Hadith 52
Narrated Aisha, Ummul Mu'minin:
The Apostle of Allah (peace_be_upon_him) said: Ten are the acts according to fitrah (nature): clipping the moustache, letting the beard grow, using the tooth-stick, cutting the nails, washing the finger joints, plucking the hair under the arm-pits, shaving the pubes, and cleansing one's private parts (after easing or urinating) with water. The narrator said: I have forgotten the tenth, but it may have been rinsing the mouth.
Muslim :: Book 2 : Hadith 498
Ibn Umar said: The Apostle of Allah (may peace be upon him) said: Trim closely the moustache, and let the beard grow.
Muslim :: Book 2 : Hadith 500
Ibn Umar said: The Messenger of Allah (may peace be opon him) said: Act against the polytheists, trim closely the moustache and grow beard.
Muslim :: Book 2 : Hadith 501
Abu Huraira reported: The Messenger of Allah (may peace be upon him) said: Trim closely the moustache, and grow beard, and thus act against the fire-worshippers.
Muslim :: Book 2 : Hadith 502
'A'isha reported: The Messenger of Allah (may peace be npon him) said: Ten are the acts according to fitra: clipping the moustache, letting the beard grow, using the tooth-stick, snuffing water in the nose, cutting the nails, washing the finger joints, plucking the hair under the armpits, shaving the pubes and cleaning one's private parts with water. The narrator said: I have forgotten the tenth, but it may have been rinsing the mouth.
Bukhari :: Book 7 :: Volume 72 :: Hadith 781
Narrated Ibn 'Umar:
Allah's Apostle said, "Cut the moustaches short and leave the beard (as it is)."

Muslim: Book 2(The Book of Purification (Kitab Al-Taharah)): Hadith 499
Ibn Umar said: The Apostle of Allah (may peace be upon him) ordered us to trim the moustache closely and spare the beard.

Tuesday, May 22, 2012

How can GOD pray?


Question:The Quran 33:56, clearly indicates that your GOD (Allah) prays, This is very strange!! How can GOD pray?

Answer:
It's true that in the Quran there is this verse
“Allah and His angels send blessings (yu-salloon) on the Prophet: O ye that believe! Send ye blessings on him, and salute him with all respect.” (Qur’an 33:56)"
It means Allah and His angels pray for Prophet Muhammad (PBUH). They argue that word ‘salah’ means ‘to pray’ so Allah according to this verse prays to someone for the Prophet (PBUH).


1- Explanation by E.W. Lane:

As to the meaning of the word in its different usages I can quote many classical Muslim authorities answering the question in extreme detail but one may say, being Muslims, they had the whole issue and all the implications, like the one suggested here, in mind and their bias may have come into play.
So let me clarify the issue using the most extensive Arabic-English lexicon compiled by a non-Muslim, Edward William Lane.

About the use of the word for Allah he writes;

And further explaining its meaning in Qur’an 33:56 where the verb is used for both Allah and the angels he says;

Edward William Lane, Arabic-English Lexicon part 4 p.444
Of particular interest is the fact that although the complete work of Lane is based on classical Muslim authorities at this point what I highlighted above is his own intake. Without citing any work he gives the meaning of ‘magnification’ to the word ‘salah’ and goes onto explain the different implications as it is used for Allah and angels. This proves it’s not the Muslim prejudice but the Arabic language which establishes the meanings current among Muslim scholars.
This is supported by what Ibn Athir, discussing various views and usages of the word, says: “It is also said that the literal origin of the word is 'to praise' and the particular worship is called 'Salah', because it entails the glorification of the Lord.” (See Nihaya fi Ghareeb al-Athar 3/95)
And this goes according to the principle;
تسمية الشئ باسم بعض ما يتضمنه
'Naming a thing for a part of it.' (See Mufradaat fi Gharaib al-Qur’an by Isfahani 1/285) As ritual prayers include ‘praising’ thus it is called Salat.
The nature of the Salat of Allah and angels is different slightly; Allah's sending His blessings on His Prophet means this: Allah is very kind to His Prophet: He praises him, blesses his work, exalts his name, and showers His mercies on him. And when it comes to angels it means: they invoke Allah’s blessings and mercy for him.


2- One verb with same meanings but slightly different implications:
A word in a passage or a sentence does not always have exactly same implication for all the subjects. For instance a person says: 'Mr. A and Mr. B helped me.' It does not necessarily mean that both helped him in exactly the same fashion. It may be that one actually did something for him and the other requested for him.

3- Meaning of ‘Salah’ when used along with ‘Rehmah’ (Qur’an 2:157):
Some try to use Quran 2:157 to prove that Salah cannot mean blessings as ‘Salah’ and ‘Rehmah’ are both used there and two words of same meaning are not used in a single sentence. But this is a twisting of the issue only. We do not say ‘salah’ means ‘mercy’ literally, infact ‘salah’ means ‘blessings’ which is a manifestation of mercy.
The word 'Salawat' (صَلَوَاتٌ) and 'Rehmah' (رَحْمَةٌ) in Quran 2:157 do not mean the same and 'salah' means 'prayer' neither. (صَلَوَاتٌ) 'Salawat,' being the plural of 'Salah', as earlier said means blessings and magnification while 'Rehmah' (رَحْمَةٌ) refers to the attribute of Mercy.
الرحمة رقة تقتضي الاحسان إلى المرحوم
'Rehmah (i.e. Mercy) is the attribute that requires being generous to the one for whom such feelings arise. (See Mufradaat fi Gharaib al-Quran 1/191)
So 'Salah' (Blessing) of Allah is because of His 'Rehmah' (Mercy) and they are not exactly the same. His 'Salah' is a manifestation of His 'Rehmah'. So the assertion that 'salah' in Quran 2:157 means 'prayers' is wrong and misleading.

4- Meaning of ‘Salah’ or ‘Rehmah’ when used along with ‘Barakah’ (Qur’an 11:73):
Yet another attempt to complicate the things made by them is discussing the word ‘Barakah’ along with ‘Salah’ and ‘Rehmah’ especially when it is used with either of them like in Quran 11:73 and the Salutations (durood) recited in ritual prayers.
Now as to the word ‘Barakah’, its meaning is:
البركة ثبوت الخير الالهى في الشئ
"Barakah in a thing shows the facilitation/ease/goodness endowed by Allah."(See Mufradaat fi Ghraib Al-Quran by Isfahani 1/44)
This also shows that Barakah is the manifestation of Allah's Rehmah (Mercy). So in Quran 11:73 it means Allah bestows his Mercy and specially Barakah, a manifestation of the same which suits the context that Allah will make their having a son at an old age easy by His Mercy which otherwise seems improbable. And in the salutations (durood) where it is used along with ‘salah’ there we pray to Allah to bestow both the manifestations of his ‘Rehmah’ on the Holy Prophet (PBUH).

5- A weak narration brought forward also supports our contention:
Then these people try to use a tradition from Ibn Kathir which they translate as:
The Israelites said to Musa: Does your Lord pray? Musa said: Fear Allah, O Sons of Israel!
Allah said: O Musa! What did your people say? Musa said: O my Lord, You already know? They said: Does your Lord pray? Allah said: Tell them My prayer for My servants is that My Mercy should precede My Anger. If it were not so, I would have destroyed them.
Firstly this tradition is not authentic according to the rules of reporting as mentioned by Albani in Silsala Ahadith Daeefa 3/387 Hadith 1388 thus it is not an evidence for us.
Secondly the last part of the narration above also belies the notion of taking ‘salah’ in the sense of supplication once used for Allah.

6- Exposing the liar, Zakariya Brutos:
‘… a very telling hadith recorded in Kitab Al Sunna by Abdullah bin Ahmad, vol.1, p.272: Apparently, when Muhammad reached the 7th heaven during the Isra and Mi'raj, he encountered Gabriel, who immediately said “Shh! Wait, for Allah is praying (Sala).” Muhammad asked: “Does Allah pray?” to which Gabriel said, “Yes, he prays.” Muhammad then asked, “What does he pray?” and Gabriel said “Praise! Praise the Lord!”’
Here Zakariya Brutos is showing his real face by corrupting the text.
Firstly he is changed the last part of the tradition which actually goes as:
قال : وما صلاته ؟ قال : يقول » سبوح قدوس رب الملائكة والروح سبقت رحمتي غضبي
"He (the Prophet PBUH) asked: 'What is His Salah?'. He (Gabriel) said, He says: 'Perfect, Most High is the Lord of the angels and the Spirit, My Mercy (Rehmah) overwhelms my wrath.'"
(Kitab Al-Sunnah by Abdullah bin Ahmad 1/468 Hadith 437)

These last words show that 'Salah' of Allah is because of His 'Overwhelming Rehmah' just as we argued above.

Do these last words give any notion of the 'prayer/supplication'? How corrupt these people are, they use a part of a tradition that suits them and change the other.
Now we venture to ask these people who are revered by Christians as ‘Fathers’ (I don’t know what that means), why the whole of the tradition was not translated as it is? Can they show us what words in the actual Arabic text of the narration have been translated as “Shh! Wait …”?
For putting the record straight let me say this narration is not authentic according to Science of Narration. For details see Silsala Ahadith Daeefa by Albani 3/386 Hadith 1387.

7- Conclusion:
a- Edward William Lane, himself a non-Muslim confirms the Muslim understanding of the word ‘salah’ when used for different subjects and that of the verse 33:56.
b- 'Rehmah', 'Salah' and 'Barakah' are related things but not exactly similar. These are subtleties of the Arabic language which may at times not be clearly differentiated in running translations for it anyway gives the general meaning correctly. Allah has used the words according to their actual meanings considering all their subtleties, as I explained 2:157 and 11:73. Translations do not clearly differentiate between their subtle differences as no language can cater for the subtleties of the other.
c- The narration from Ibn Kathir and Abdullah bin Ahmad they quote, though of dubious authority, belies their own argument.
d- And most importantly it exposes the liars whom certain Christians recognize as their religious leader. We can only sympathize for those whose supposed-to-be spiritual guides are liars. May Allah have mercy on them!
Animated Social Gadget - Blogger And Wordpress Tips Twitter Bird Gadget