Saturday, May 5, 2012

Kwanini waislamu mnasema maandiko ya biblia yanahitilafu?

Swali:
Kwanini waislamu mnasema maandiko ya biblia yanahitilafu?



Jibu:
Yafuatayo ni mahitlifiano ya maandiko katika biblia.

Michael binti wa Saul hakupata mtoto mpaka kifo chake.(2 samweli 6:23)
Michael binti wa Saul alikuwa na wavulana watano (2 Samweli 21:8)

Benjamin alikuwa na watoto watatu. (1 Mambo ya Nyakati 7:6)
Benjamin alikuwa na watoto watano. (1 Mambo ya Nyakati 8:1-2.

Harun alikufa huko Hor. (Hesabu 33:38)
Haruni alikufa huko Mosera (Kumb. 10:6)

Yehoremu alishikilia kutawala wakati akiwa na umri wa mika 32 alifariki katika miaka 40,(2 Mambo ya Nyakati 21:5) (2 Mambo ya Nyakati 21:20).
Baada ya kifo chake mtoto wake mdogo alishikilia serikali na alikuwa na umri wa miaka 42 wakati ule.(2 Mambo ya Nyakati (22:1-2).
Kana kwamba mwana mdogo alikuwa miaka miwili zaidi kuliko baba mzazi! (9. Mat 5:17; Mat 5:38-40; Hebrew 7:12).


Sungura hucheua (Mambo ya Walawi 11:6). Lakini ukweli ni kwamba Sungura hacheui kabisa.

Yuda aliyemsaliti Yesu alivitupa vile vipande vya fedha alivyopewa kwa udhalimu wake huo, kisha alijinyonga na
wakuu wa Makuhani wakavichukua vipande vya fedha na wakanunulia shamba la kuzikiwa watu (Mat 27:5-7).
Lakini (Matendo 1:18), inasema kwamba Yuda mwenyewe alinunua konde kwa ijara aliyoipata kwa udhalimu wake huo na kisha akaanguka na kupasuka na matumbo yake yote yakatoka.

Yesu alifyolewa na wanyang’anyi wawili aliposulubiwa pamoja nao. (Marko 15:32 ; Mat. 27:44).
Lakini katika Luka 23:39-40, inasema kuwa mnyang’anyi mmoja ndiye aliyemfyolea Yesu.

Yuda alijinyonga.(Mat. 27:5).
Lakini katika Matendo 1:18, imeandikwa kwamba alianguka na kupasuka matumbo yake

Mwanadamu aliumbwa baada ya uumbaji wa wanyama.(Mwanzo 1:25-26).
Lakini katika (Mwanzo 2:18-20), inaonekana mwanadamu aliumbwa kwanza.

Mwandishi wa Torati siye Nabii Musa mwenyewe.
Basi Musa mtumishi wa bwana akafa huko katika nchi ya Moabu kwa neno la Bwana. (Kumb. 34:5).

Mwandishi wa Kitabu cha Mathayo si Mathayo mwenyewe ambaye ni mwanafunzi wa Yesu.(Mat. 9:9).

No comments:

Post a Comment

Animated Social Gadget - Blogger And Wordpress Tips Twitter Bird Gadget